Skip to main content

Baada ya maandamano

BAADA YA MAANDAMANO.
Imeamdaliwa: GLEN DON 
Katiba humu nchini inaruhusu kuwepo kwa maandamano ila iwe maandamano ya amani yasiyo na uchochezi, ghasia wala uhalifu.

Leo ni siku ya tatu ya maandamano tangu Mheshimiwa Raila Odinga kutangaza maandamano hayo kufanyika mara tatu kwa wiki mfululizo ikiwa ni; Jumatano, Alhamisi na Ijumaa.

Maandamano hayo ni ya kupinga bajeti ya mwaka wa fedha ya 2023/24 na pia kushinikiza serikali kupunguza gharama na hali ya maisha magumu yanayokumba wananchi.

Bwana Odinga anahisi kuwa serikali inafanya kazi duni kupunguza gharama ya maisha.
Njia hii ya maandamano ilibuniwa na wanasiasa wa Azimio wakiongozwa na Bwana Odinga ili kufikisha ujumbe nzito kwa serikali.
Tangu maandamano hayo yaanze, serikali haipinduki wala hawatikiswi, je tunaweza sema kuwa maandamano hayana ujumbe au ni serikali kichwa ngumu na haitaki kusikiliza malalamishi ya wananchi?

Bwana Odinga ni miongoni mwa shujaa ambao walitetea sana hapo awali demokrasia, ustawi wa uchumi, na pia kuwepo huru nchini Kenya.
Iweje baadhi ya maendeleo haya leo yanapitia majaribu mikononi mwa waandamanaji.
Kila siku ndani ya waandamanaji kuna wale wachochezi, wahalifu, na wenye tendo la ugaidi vilevile kuna wale waandamanaji halali wale wanaoandamana juu ya hali gumu ya maisha, pia kuna wale wanao tii sheria na kauli za Bwana Odinga kwani 'Baba' akisema kulia au kushoto ni hivyo.
Kila mara watu wanapo andamana lazima wawe watu hawa watatu.
Mioto zinawakizwa barabarani, mali kuharibiwa kama ile tukio ya Mlolongo Machakos, uporaji wa mali kwa hali ya utata, kando na hayo maisha yanapotezwa.

Tangu maandamano yaanze inakadiriwa kuwa vifo vya watu isiyopungua 30 vimetokea na makumi ya watu kuumia kutokana na ghasia ya maandamano, cha kutikitisha ni kuwa mauaji na majeraha haya yanasababishwa na wanapolisi, Swali ni Je Serikali inatumia nguvu kupita kiasi au ni waandamanaji Wana ugumu wa kuelewa jukumu lao wanapo andamana? Pengine ni vibaya kukata hukumu shingo upande, na tusitumie mate wino ungalipo.

BAADA YA MAANDAMANO
 Tunapochoma lami na kupora mali ya Wakenya wenzetu, je tumezika wapi fikra zetu?

Lazima tujue kuna maisha baada ya maandamano.
Barabara zinapochomwa na mali zinapoporwa ni taswira mbaya tunayoonyesha.
Kuna njia mbadala ya kuashiria ghadhabu tunapoandamana.
Tunapo washa moto kwenye barabara zetu, ni maendeleo tunarejesha nyuma, tunapo pora mali ya Wakenya wenzetu ni chuki tunaeneza.

Sisi ni Wakenya wazalendo, katika wimbo wetu wa taifa tunahimizwa kupitia wimbo huo, kuwa tuishi kwa amani, na tunapotenda matendo yanayokinzana na mistari za wimbo wetu wa taifa, je huo ni uzalendo?
Kwa hakika, maandamano yamekubaliwa na katiba yetu, pia panapofanyika maandamano viongozi huwa hawana amani na wanaibishwa mno, Kwa hivyo wazo la fikra ni je Bwana Ruto anaweza kimya tu hivyo anapoona hayo yote yakifanyika?

Kuna Maisha baada ya maandamano.
Kuna amani baada ya maandamano, ndiyo tunafaa kudumu ndani ya upendo na umoja.
Tunapoeneza chuki, swali tunalofaa tujiulize kimawazo ni, je jirani wangu kesho ataweza kuniazimu maji ya kunywa, ata tone tu la kuua tama? Je nitaweza kusafiri popote nchini kwa amani? Ninasisitiza kuwa kuna Maisha baada ya maandamano.
Yaliyojengwa miongo kadhaa tusiyabomoe kwani kuna maisha ya kuishi baada ya maandamano na tutayategemea. Tusibomoe daraja baada au kabla ya kuvuka bahari kwani kesho pia ni siku.
Tusiwadharau mashujaa waliopigania uhuru wa taifa letu, waliopigania uchumi wetu. Kazi nzuri waliofanya tusije tukayazike.
Njia bora ni kulinda kazi waliozifanya kwa kuwa kuna maisha baada ya maandamano.
Idadi kubwa ya waandamanaji ni vijana, na wazee ni nadra sana kupata.
Tunavyojua ujana ni moshi, na uzee hauepukiki, kesho tukisha zeeka, tutaambia wajukuu na watukuu nini?
Tutawaambia nini, ikiwa tunazungumza lugha moja na hakuna amani, upendo na umoja? Ikiwa maendeleo hayatakuwa na fursa tulikuwa nazo sote? 
Kuyajenga yaliyoharabiwa kwa hakika si rahisi,
Maandamano ya mwaka huu si ya kwanza, ya hapo awali maafa yalitokea na haki ingali kutimizwa, pia tukumbukeni kuwa maisha yaaja mara moja na hayawezi kukarabatiwa wala marejesho hayako.
Tutamlilia nani aje ajenge barabara, tutapata wapi pa kustawisha biashara zetu siku zijazo.
Kuna Maisha baada ya maandamano.
Wakati majirani wetu wanaendelea kufanya kazi nasi tupo barabarani keshoye ikifika tutasema nini wakitucheka.
Tunayo maisha baada ya maandamano na ni jukumu letu kuweka maisha hayo yawe ya maana na dhamana.

KUNA MAISHA YA KUISHI.
Kila siku tujue ya kwamba " maji mtoni hayasubiri mwenye kiu."

Kwa: WANANCHI WAZALENDO 

 EAGLE'S 🦅 EYE 👁️ (JICHO LA TAI)

Comments

Popular posts from this blog

SINGAPORE AND KENYA: DAY AND NIGHT

Kenya got its independence 1963 from the British colony, while Singapore got it two years in the month of August 9, 1965 from Malaysia after they had intense political differences which resulted to racial riots. Standing on the mirror line reflecting on the two countries between Kenya and Singapore, Kenya is extremely behind Singapore in terms of development.  Singapore hastily rose from third world country to first world country while Kenya still maintained the third world class.  Recently, Kenya's President Dr. William Ruto, is full of comparison statements: between Kenya and Singapore. Surprisingly, the phrase of boosting Kenya's world class has taken a beautiful twist where every politician is dreaming of Kenya to be futuristically the same level as Singapore. Pausing a bit, what's a dream? pondering on this; a dream literally means imaginary events while sleeping.  Our politicians are forgetting the dogmatic saying that goes 'action speaks louder than...

THE CHANGE EXPECTED IN REVERSE: GEN Z'S FADING STRENGTH

Photo Courtesy   Waking up to find the sun rising from the West and not East at dawn is enough to signal a whirl of change in the cosmological history. As a product of imagination it can be, who knew Gen Z would emerge as with a wave of change in a sundry of generations unexpectedly.  With this wave, the political sphere in every country worldwide is experiencing an overhaul.  Recently, protests have marred different countries with calls for change.  Bangladesh, Nepal, Morocco, Madagascar, Kenya are some of the countries that have at least tasted the pinch of the GenZ protests, while some of the protests have resulted in a change in the political sphere of the affected countries others have left less impact with mission and vision unreached due to fanciful impulse.  Generation Z, globally have not only expressed their anger through anger through protests and demonstrations, but also in politics where some of the African countries like Seychelles and...

NOT-NOW: HAVE SOME HUMANITY

photo courtesy (unknown) A person cannot retract a message that has reached a mass audience invariant of where it was said. One of the characteristics of communication is that you cannot uncommunicate.  A silent person remains wise until he utters a word. His Excellency Mutahi Kahiga might exemplify this phrase considering his tracenda during his speech at a funeral in Kiambu county, where he was addressing them in the local dialect.  Mr. Kahiga, seems to be deficient in emotions especially concerning the latest tragedy that befell the country when he cast aspersions on Raila Odinga's demise.  Raila Odinga, without doubt was akin to mumbo-jumbo within the luo community yet to his capacity during his lifetime did he not only benefit the Luo but became a national figure and perhaps a trademark in Kenya's politics.  In the history of human life, man is mortal and from soil we come, to soil shall we return. Regardless of the circumstances, man is...