Skip to main content

Baada ya maandamano

BAADA YA MAANDAMANO.
Imeamdaliwa: GLEN DON 
Katiba humu nchini inaruhusu kuwepo kwa maandamano ila iwe maandamano ya amani yasiyo na uchochezi, ghasia wala uhalifu.

Leo ni siku ya tatu ya maandamano tangu Mheshimiwa Raila Odinga kutangaza maandamano hayo kufanyika mara tatu kwa wiki mfululizo ikiwa ni; Jumatano, Alhamisi na Ijumaa.

Maandamano hayo ni ya kupinga bajeti ya mwaka wa fedha ya 2023/24 na pia kushinikiza serikali kupunguza gharama na hali ya maisha magumu yanayokumba wananchi.

Bwana Odinga anahisi kuwa serikali inafanya kazi duni kupunguza gharama ya maisha.
Njia hii ya maandamano ilibuniwa na wanasiasa wa Azimio wakiongozwa na Bwana Odinga ili kufikisha ujumbe nzito kwa serikali.
Tangu maandamano hayo yaanze, serikali haipinduki wala hawatikiswi, je tunaweza sema kuwa maandamano hayana ujumbe au ni serikali kichwa ngumu na haitaki kusikiliza malalamishi ya wananchi?

Bwana Odinga ni miongoni mwa shujaa ambao walitetea sana hapo awali demokrasia, ustawi wa uchumi, na pia kuwepo huru nchini Kenya.
Iweje baadhi ya maendeleo haya leo yanapitia majaribu mikononi mwa waandamanaji.
Kila siku ndani ya waandamanaji kuna wale wachochezi, wahalifu, na wenye tendo la ugaidi vilevile kuna wale waandamanaji halali wale wanaoandamana juu ya hali gumu ya maisha, pia kuna wale wanao tii sheria na kauli za Bwana Odinga kwani 'Baba' akisema kulia au kushoto ni hivyo.
Kila mara watu wanapo andamana lazima wawe watu hawa watatu.
Mioto zinawakizwa barabarani, mali kuharibiwa kama ile tukio ya Mlolongo Machakos, uporaji wa mali kwa hali ya utata, kando na hayo maisha yanapotezwa.

Tangu maandamano yaanze inakadiriwa kuwa vifo vya watu isiyopungua 30 vimetokea na makumi ya watu kuumia kutokana na ghasia ya maandamano, cha kutikitisha ni kuwa mauaji na majeraha haya yanasababishwa na wanapolisi, Swali ni Je Serikali inatumia nguvu kupita kiasi au ni waandamanaji Wana ugumu wa kuelewa jukumu lao wanapo andamana? Pengine ni vibaya kukata hukumu shingo upande, na tusitumie mate wino ungalipo.

BAADA YA MAANDAMANO
 Tunapochoma lami na kupora mali ya Wakenya wenzetu, je tumezika wapi fikra zetu?

Lazima tujue kuna maisha baada ya maandamano.
Barabara zinapochomwa na mali zinapoporwa ni taswira mbaya tunayoonyesha.
Kuna njia mbadala ya kuashiria ghadhabu tunapoandamana.
Tunapo washa moto kwenye barabara zetu, ni maendeleo tunarejesha nyuma, tunapo pora mali ya Wakenya wenzetu ni chuki tunaeneza.

Sisi ni Wakenya wazalendo, katika wimbo wetu wa taifa tunahimizwa kupitia wimbo huo, kuwa tuishi kwa amani, na tunapotenda matendo yanayokinzana na mistari za wimbo wetu wa taifa, je huo ni uzalendo?
Kwa hakika, maandamano yamekubaliwa na katiba yetu, pia panapofanyika maandamano viongozi huwa hawana amani na wanaibishwa mno, Kwa hivyo wazo la fikra ni je Bwana Ruto anaweza kimya tu hivyo anapoona hayo yote yakifanyika?

Kuna Maisha baada ya maandamano.
Kuna amani baada ya maandamano, ndiyo tunafaa kudumu ndani ya upendo na umoja.
Tunapoeneza chuki, swali tunalofaa tujiulize kimawazo ni, je jirani wangu kesho ataweza kuniazimu maji ya kunywa, ata tone tu la kuua tama? Je nitaweza kusafiri popote nchini kwa amani? Ninasisitiza kuwa kuna Maisha baada ya maandamano.
Yaliyojengwa miongo kadhaa tusiyabomoe kwani kuna maisha ya kuishi baada ya maandamano na tutayategemea. Tusibomoe daraja baada au kabla ya kuvuka bahari kwani kesho pia ni siku.
Tusiwadharau mashujaa waliopigania uhuru wa taifa letu, waliopigania uchumi wetu. Kazi nzuri waliofanya tusije tukayazike.
Njia bora ni kulinda kazi waliozifanya kwa kuwa kuna maisha baada ya maandamano.
Idadi kubwa ya waandamanaji ni vijana, na wazee ni nadra sana kupata.
Tunavyojua ujana ni moshi, na uzee hauepukiki, kesho tukisha zeeka, tutaambia wajukuu na watukuu nini?
Tutawaambia nini, ikiwa tunazungumza lugha moja na hakuna amani, upendo na umoja? Ikiwa maendeleo hayatakuwa na fursa tulikuwa nazo sote? 
Kuyajenga yaliyoharabiwa kwa hakika si rahisi,
Maandamano ya mwaka huu si ya kwanza, ya hapo awali maafa yalitokea na haki ingali kutimizwa, pia tukumbukeni kuwa maisha yaaja mara moja na hayawezi kukarabatiwa wala marejesho hayako.
Tutamlilia nani aje ajenge barabara, tutapata wapi pa kustawisha biashara zetu siku zijazo.
Kuna Maisha baada ya maandamano.
Wakati majirani wetu wanaendelea kufanya kazi nasi tupo barabarani keshoye ikifika tutasema nini wakitucheka.
Tunayo maisha baada ya maandamano na ni jukumu letu kuweka maisha hayo yawe ya maana na dhamana.

KUNA MAISHA YA KUISHI.
Kila siku tujue ya kwamba " maji mtoni hayasubiri mwenye kiu."

Kwa: WANANCHI WAZALENDO 

 EAGLE'S 🦅 EYE 👁️ (JICHO LA TAI)

Comments

Popular posts from this blog

THE UNSINKABLE THAT SUNK

By Glen Don  112 YEARS GONE  In the Atlantic ocean one of the horrible things happened. Lives were lost, property of invaluable destroyed and other belongings got lost. It is exactly a hundred and twelve years since 'The Unsinkable' sunk and never to be resurfaced on water or on earth. The Titanic ship during the time would be the largest ship on earth to be ever built, The Titanic ship during its era of the launch was the largest in the world. The ship's capacity is said to be possibly 3,300 while those who were on board is said to be about 2,000 and of those who boarded only thirty two percent survived the shipwreck. Majority of those who survived were women and children. This is due to the privilege they were granted to be the first people to be saved. The Titanic ship shipwrecked after hitting an iceberg that was ahead of it, due to the surcharged pressure, the ship divided into two making it to get submerged in the Atlantic ocean. The ship sunk down the ocean when it ...

The Room of two contradicting speeches

The miss link in communication in the Government as a unit is a puzzle. President William Ruto was today on May 3, expected to address the nation on the state of the nation in regard to the flood. Just before the President addressed the nation, there was a memo circulating already of how the school reopening would go on as planned. The Ministry of Education while addressing the safety of the learners through the memo directed that the School Board of Management to ensure that the learners are ready for learning and precautionary measures are undertaken to avoid hindrances. Later, two hours after the memo, the President addressed the nation and ordered that the postponement of school reopening be suspended until further notice. Out of the impossible, the ministry of education seemed to be having the stand of opening schools. The Education Cabinet Secretary seems to be under pressure when he was releasing the memo since the last was released on the wee hours of the morning hence today...

KENYA'S SMARTPHONE COMPANY TO WELCOME

 EAST AFRICA DEVICE ASSEMBLY LIMITED KENYA The President yesterday Monday 30, launched an industry that will manufacture Kenya-made smartphones.  The phones are expected to be selling at Ksh. 7,500 higher price compared to the initial price that was earlier said by the President His Excellency Dr William Ruto which was ksh. 5,000. If the company starts to run, then it will be the Kenya's first industry to perform such task. The smartphones are expected to be unleashed to the market in about less than a year. The phones will be available in Faiba shops, and Safaricom shops among other authorised dealers by the Government. The types of brand names will be Neon, and Smarta. The president also said that the gadgets will be available in installments.  This is the best point for Kenya to start for even a journey of one thousand miles starts with a step.  Could be the smartphone an individual's interest or it is out of goodwill, this a puzzle worth not be solved now. The pa...